Swahili: Open Bible Stories

Updated ? hours ago # views See on DCS

30. Yesu Anawalisha Watu Elfu Tano

OBS Image

Yesu aliwatuma mitume kuwahubiri na kuwafundisha watu vijiji tofauti, nao waliporudi kwa Yesu, waka mueleza kile walicho fanya, Yesu akawaalika kwenda faragha ng'ambo ya mto kwa mapunziko, nao wakapanda mashua kuelekea ng'ambo ya mto.

OBS Image

Lakini walikuwako watu wengi waliomuona Yesu na wanafunzi wakaondoka kwenye mashua, Watu walipita pembezoni mwa ziwa kuelekea upande wa pili mbele yao, hivyo Yesu na wanafunzi wake walipowasili, tayari kundi kubwa la watu walikuwako huko wakiwasubili.

OBS Image

Umati ulikuwa zaidi ya wanaume 5000 bila kuhesabu wanawake na watoto, Yesu aliona mkutano mkubwa mbele yake nao walikuwa kama kondoo waliokosa mchungaji, kwa hiyo akawafundisha na kuwaponya watu miongoni mwao ambavyo walikuwa wagonjwa.

OBS Image

na ilipokuwa jion wanafunzi walimwambia Yesu, tumechelewa na hakuna mji karibu, basi uwaage watu ili waweza kwenda kujitafutia kitu wale.

OBS Image

Yesu akawaambia wanafunzi, "mnaweza kuwapatia chochote wale!" wakamjibu ni vipi tunaweza kufanya hivyo? sisi tuna vipande vitano vya mkate na samaki wawili

OBS Image

Yesu akawaambia wanafunzi wa waambie watu kwenye umati wakae chini kwenye nyasi kwa makundi ya watu 50

OBS Image

Na Yesu akachukua vile vipande vitano vya mikate na samaki wawili, akatazama mbinguni akamshukuru Mungu kwa Chakula.

OBS Image

Kisha Yesu akaigawa mikate na samaki vipande, akawapatia vile vipande wanafunzi wawagawie watu. Wanafunzi wakaendelea kupita nje na chakura, wala hakikuisha, watu wote wakala na kutosheka.

OBS Image

Baada ya hapo wanafunzi walikusanya mabaki ya chakula, navyo vilikuwa vikapu kumi na mbili, nacho chakula chote kilitokana na Mikate mitano na Samaki wawili.

Simulizi ya Biblia kutoka: Matayo14:13-21; Marko 6:31-44; Luka 9:10-17; Yohana 6:5-15