01-01
Mwanzo
Huu ni, "mwanzo wa vitu vyote" kabla ya kuwepo kitu chochote isipokuwa Mungu.
Aliumba
Hapa inatumika kumaanisha kutengeneza kitu pasipokutumia kitu.
Ulimwengu
Hii inajumuisha kila kitu ambacho Mungu aliumba duniani na mbinguni, vyote vinavyo onekana na visivyo onekana.
Dunia
Neno "Dunia" linamaanisha ulimwengu wote ambao watu wanaishi.
Giza
Giza maana yake kutokuwepo na mwanga kabisa, kwasababu Mungu alikuwa bado hajaumba mwanga.
Utupu
Mungu bado hajaumba kitu chochote isipokuwa Dunia iliyofunikwa na maji.
Hakuna kilichokuwa kimeumbwa
Hapakuwepo na uumbaji wa vitu isipokuwa maji iliyofunika dunia.
Roho wa Mungu
Roho wa Mungu, wakati mwingine huitwa Roho Mtakatifu, alikuwepo toka mwanzoni, alitembea juu ya dunia ili aumbe vyote alivyo kusudia.
01-02
Mungu akasema
Mungu aliumba mwanga kwa kutamka neno.
Na iwe
Hii ni amri iliyotokea mara moja kwasababu ilinenwa na Mungu. Inaweza kutafsiriwa kwa njia ya kawaida kuwa ni neno lenye uhakika wa kutokea. Kwa mfano, unaweza kutafsiri kama, "Mungu akasema, 'Pawepo na Mwanga.'"
Mwanga
Huu ni mwanga maalum ambao Mungu aliumba-jua halikuumbwa hadi baadaye.
Ikawa nzuri
Maneno haya yalitumika mara kwa mara katika historia ya uumbaji, na kusisitiza kuwa kila hatua ya uumbaji ilikuwa ikimpendeza Mugu na kutimiza mipango na kusudi lake.
Uumbaji
Neno hili limetumika hapa kumaanisha siku sita ambazo Mungu alivifanya vitu vyote vilivyoko.
01-03
Siku ya pili
Kazi za Mungu za uumbaji ulifuata utaratibu, makusudi na mpangilio. Vitu alivyoumba kwa kila siku zilijenga na kutegemea vitu vya siku iliyotangulia.
Mungu akasema
Mungu aliumba anga kwa kusema neno.
Kuumba
Mungu aliumba anga pasipokuwepo na kitu.
Anga
Neno hili linamaanisha sehemu yote ya juu ya Dunia, hii ikiwa ni pamoja na hewa tunayovuta na mbingu.
01-04
Siku ya tatu
Ni siku iliyofuata kwenye mtiririko ambapo Mungu aliandaa Dunia kwa Maisha.
Mungu akasema
Mungu aliumba nchi kavu kwa kuamuru.
dunia
neno hili limetumika kumaanisha sehemu vumbi au udongo, ambayo ardhi iliyo kavu imetegenezwa.
Kuumba
Neno hili linatumika kumaanisha, kutengeneza kitu pasipo kutumia kitu chochote.
01-05
Mungu akasema
Mungu aliumba mimea yote kwa kuamuru.
Nchi na izae
Hii ni amri iliyotokea mara moja kwa sababu Mungu alinena.
Aina zote
Hii ni aina mbali mbali ya mimea na miti.
Kuumba
Neno hili linatumika kumaanisha, kutengeneza kitu pasipo kutumia kitu chochote.
Kilikuwa chema
Neno hili limetumika mara nyingi katika historia ya uumbaji, hii ikisisitiza ya kuwa kila hatua ya uumbaji ilimpendeza Mungu na kutimiza lengo na kusudi yake.
01-06
siku ya nne
Ni siku ilyofuata kwa mpangilio wa uumbaji wa siku ambayo Mungu aliumba.
Mungu akasema
Mungu aliumba jua, mwezi, na nyota kwa kuamuru.
mwanga
Ni kitu ambacho kinang'aa angani na kutoa mwanga kwa dunia.
usiku na mchana, nyakati na miaka
Mungu aliumba mianga tofauti tofauti ili kutofautisha sehemu ya muda kuanzia ndogo hadi kubwa, na kuziweka zijirudia kwa wakati wote hadi mwisho wa wakati.
Kuumba
neno hili linatumika kumaanisha, kutegeneza kitu pasipo kutumia kitu chochote.
01-07
siku ya tano
Mungu aliendelea na mpangilio wake wa uumbaji ambayo alianza siku nne zilizopita.
Mungu akasema
Mungu aliziumba ndege na vitu viishivyo majini kwa kuamuru.
Kila kiumbe kinacho ishi na kwenda majini
Mungu hakuumba tu samaki, bali kila aina ya viumbe vyenye kuishi na kwenda ndani ya maji. Kila mmoja anaishi kwa sababu Mungu alichagua kuumba.
ndege wote
Mungu hakuumba tu aina moja ya ndege, lakini aliumba aina mbalimbali za ndege wazuri ajabu wenye kutofautiana maumbo, ukubwa na rangi.
ni vyema
Neno hili limetumika mara nyingi katika histora ya uumbaji, hii ikisisitiza kuwa kila hatua ya uumbaji ilikwenda kama ilivyokusudiwa kutokana na mpango wa hekima ya Mungu na kusudi lake.
aliwabariki
Mungu aliongea nia yake kuwa wangebarikiwa na kwamba mambo yao yote yaengekwenda vema katika dunia aliowaweka.
01-08
siku ya sita
Jambo lililofuata, mpangilio katika mfuatano wa siku za matendo ya uumbaji.
Mungu akasema
Neno alilo liongea Mungu ndiyo njia ambayo wanyama waliumbwa.
aina mbambali
Hii inamaanisha vitu vingi tofauti tofauti, lakini vyenye mpangilio.
wanyama wa nchi
Ni aina mbalimbali ya wanyama walioishi juu ya aridhi, mbali na ndege, au wanyama walioishi majini.
wanyama wa shambani
Ni aina ya wanyama wanaishi kwa amani na watu juu ya ardhi, kwa jina lingine ni wale wanyama wa kufugwa.
wanaotambaa juu ya nchi
Hii inajumisha jamii ya wanyama wote watambaao kama reptilia na wadudu.
porini
Ni aina ya wanyama ambao mara nyingi hawaishi kwa amani na watu, hii ni kwa sababu wanaogopa watu, au ni hatari kwao.
ni vyema
Neno hili limetumika mara nyingi katika histora ya uumbaji, hii ikisisitiza kuwa kila hatua ya uumbaji ilikwenda kama ilivyokusudiwa kutokana na mpango wa hekima ya Mungu na kusudi lake.
01-09
Na tumfanye
Hii inaonyesha makusudi ya Mungu, kufanya maamuzi ya kumtengeneza mtu kwa namna ya aina yake na kwa makusudi fulani. Inawezekana kutafsiriwakama, "Tutafanya."
Sisi...yetu...sisi
Biblia inafundisha kuwa kuna Mungu mmoja, lakini kwa maneno ya Agano la Kale "Mungu" iko katika neno la wingi. Na Mungu hutumia maneno ya wingi pale anapoongelea juu yake. Wengine wanafahamu hii kama njia maalumu ya kuelezea ukuu wa Mungu, na wengine hufahamu hii kama Mungu Baba akiongea kwa Mwanaye na Roho Mtakatifu, ambao wote ni Mungu.
kwa mfano wetu
Mfano, ni taswira inayowakilisha sura ya kitu halisi au mtu. Watu walifanywa kwa namna ambayo wanaweza kuonyesha na kuwakilisha baadhi ya tabia na sifa za Mungu.
kama sisi
Watu wanazishriki baadhi ya tabia za Mungu ila siyo tabia zote. Maneno haya yanaweza kutafsiriwa kuwa mwanadamu anafanana na Mungu, ila hayuko sawa na Mungu na au jinsi alivyo.
mamlaka
Mungu aliwapa watu uhuru na nguvu ya kutawala, kuongoza na kuamua namna dunia na wanyama watakavyotumika.
01-10
alichukua vumbi
Mungu alimfanya mwanadamu kwa kutumia mavumbi kutoka ardhini. Neno hili pengine linaweza kuwa tofauti na neno lililotumika mara kwa mara la neno dunia.
alimfanya
Neno hili linaonyesha kuwa Mungu mwenyewe alimtengeneza mwanadamu. Hii ni sawa na mwanadamu anavyo tengeneza kitu kwa mikono waye mwenyewe. Hakikisha neno lingine tofauti na "uumbaji" linatumika, hii ni tofauti na alivyo umba vitu vingine vyote ambavyo alifanya hivyo kwa kuamuru kwa kutamka tu.
mtu
Kwa wakati huu aliyetengenezwa ni mwanaume tu, mwanamke alitengenezwa baadaye kwa njia nyingine.
akampulizia uhai
Neno hili inaonyesha Nafsi ya Mungu, tendo la ukaribu la kuhamisha uhai wake kwenda kwenye mwili wa Adamu, linganisha na namna mtu anavyotoa hewa.
uhai
Katika tendo hili, Mungu alimpulizia mwanadamu uhai wa mwili na roho ndani ya mtu.
adamu
Jina la adamu ni sawa na neno katika agano la kale lenye maana ya "mtu" na ni sawa na neno la udongo/mavumbi ambao alifanywa kwayo.
bustani
Ni eneo la ardhi lililopandwa miti na mimea kwa kusudi-mara nyingi kuzalisha chakula au kufanya sehemu kuwa nzuri.
aitunze
Kuendeleza bustani kwa kulimia, kupalilia, kunyeeshea, kuvuna, kupanda n.k.
01-11
katikati
Sehemu ya katikati hutia mkazo na umuhimu wa miti hizo miwili.
bustani
Ni eneo la ardhi lililopandwa miti n amimea kwa kusudi -mara nyingi kuzalisha chakula au kufanya sehemu kuwa nzuri.
Mti wa uzima
Mtu alaye matunda katika mti huu hatakufa kamwe.
mti wa ujuzi wa mema na mabaya
Matunda ya mti huu humuwezesha mtu kutambua mema na mabaya.
ujuzi
Kuelewa au kufahamu kwa kuwa na uzoefu nao.
mema na mabaya
Mabaya ni kinyume cha mazuri. Kama ambavyo mazuri humaanisha yale mazuri yanayompendeza Mungu, mabaya humaanisha kitu chochote ambacho hakimpendezi Mungu.
kufa
Katika hali hii, atakufa kimwili na kiroho.
01-12
siyo vema
Hii ni mara ya kwanza katika uumbaji kwa kitu kutokuwa kizuri. Ina maanisha "bado haijawa nzuri" kwa sababu Mungu hajamaliza kazi ya kumuumba mwanadamu.
peke yake
Adamu alikuwa mwanadamu mwenyewe, pasipo kuwapo na nafasi ya kuwa na uhusiano na mwanadamu mwingine. Na hakuweza kuwazaa watoto na kuongezeka.
Msaidizi wa Adamu
Hapakuwepo yeyote aliyefanana kiasi cha Adamu kuweza kuungana naye kukamilisha shughuli alizopewa na Mungu. Hakuna mnyama awezaye kufanya havyo.
01-13
usingizi mzito
Huu ulikuwa usingizi usio wa kawaida.
akatoa ubavu mmoja na kutengeneza
Maneno haya, yanaonyesha kitendo cha Mungu kutoa ubavu wa Adamu na kutengeneza mwanamke.
mwanamke
Alikuwa mwanamke wa kwanza, mwanadamu mwenye jinsia ya kike ambaye alikuwa hajatengenezwa hadi wakati ule.
akamleta kwake
Ni Mungu mwenyewe ndiye aliyewatambulisha. Alimleta Mwanamke kwa Adamu, kama kutoa zawadi nzuri kwake.
01-14
Hatimaye!
Adamu alisema hivyo kuonyesha kuwa alikuwa akisubiri kitu kama mwanamke.
Kama mimi
Mwanamke alikuwa ni mwanadamu kama Adamu, pamoja na kwamba kulikuwepo na tofauti za umuhimu kati yao.
Mwanamke
Neno hili linamanisha muundo wa kike ambayo siyo mwanaume.
kutengenezwa kutokana na mwanaume
Mwanamke alitengenezwa kutokana na mwili wa Adamu.
mwanaume atamuacha
Hii ilitamkwa kwa wakati uliopo ili kuonyesha mwenendo utakao kuwepo katika siku za baadaye. Adamu alikuwa hana mama wala baba, lakini wanaume wengine wote watakuwa nao.
watakuwa mmoja
Mme na mke watashirikiana katika mahusiano ya karibu na kipekee, katika umoja na kujitoa kwa kila mmoja wao kwa mahusiano yanayozidi mahusiano na watu wengine wote.
01-15
Mungu alimtengeneza
Mungu alimtengeneza mwanaume na mwanamke kwa namna ya kipekee.
kwa sura yake
Taswira au sura ni kiwakilishi halisi cha kitu au mtu. Mungu aliwatengeneza watu ili kuonyena na kuwakilisha baadhi ya tabia na sifa za Mungu, lakini siyo kuwa sawa na yeye.
chema sana
Hii inaonyesha zaidi ya maneno yaliyotumika hapo nyuma ya kama ni chema, vyema. Chema sana inamaanisha kwa uumbaji wote na siyo to kwa mwanaume na mwanamke. Kila kitu ilikuwa sawasawa na kama Mungu alivyokitaka kiwe.
Uumbaji
Siku sita ambazo Mungu alitumia kuumba kila kitu.
01-16
siku ya saba
Ni siku iliyofuata baada ya siku ya sita kuisha.
amemaliza kazi yake
Mungu alimaliza kazi ya uumbaji ila bado anafanya kazi zingine.
Mungu akapumzika
Mungu "alipumzika" kwa sababu kazi ya uumbaji ulikamilika. Mungu hakuchoka, au si kwamba ameshindwa kuendelea.
Aliibariki siku ya saba
Mungu alikuwa na mpango nzuri maalum kwa siku ya saba, na kwa kila siku ya saba baadaye.
akaifanya takatifu
Hii ina maana, "Mungu alitenga" siku hii kama siku maalum. Haitatumika kama siku nyingine za wiki.
ulimwengu
Hii inajumuisha kila kitu alihoumba Mungu hapa duniani na mbinguni, yale yanayo onekana na yasiyo onekana.