Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

36-01

Siku moja

Kipengele hiki kinatambulisha tukio ambalo lilitokea kipindi kilichopita, lakini halielezi muda maalumu. Lugha nyingi huanza kuelezea habari ya kweli kwa njia inayofanana.

Yakobo

Huyu ni Yakobo tofauti na yule aliyeandika Kitabu cha Yakobo kwenye Biblia. Kwa kuweka wazi hili, baadhi ya lugha zinaweza kuhitaji kidogo kutumia majina tofauti mawili au kutofautisha kulitamka.

36-02

Kitu cheupe

Hiki ni , "cheupe zaidi" pia kinaweza kutafsiriwa kama nuru (chanzo cha mwanga) au angavu

36-03

iliyoonekana

Vilevile inawezekana kusema, "ilionekana bila kujua ilikotokea." Ghafla walikuwa pale au, walitokea kwa ghafla.

kifo chake, ambacho kingetokea karibuni

Hii inaweza kutafasiriwa kama, "jinsi atakavyo kufa karibuni" au, "jinsi ambavyo wangemuua muda si mrefu"

ndani ya Yerusalemu

Baadhi ya lungha zinaweza kupendelea kusema, "katika jiji la Yerusalemu."

36-04

vibanda

Hii vilevile inaweza kutafasiriwa kama, "kivuli" au vibanda vya bustanini" au, hema. Hii inarejea kwenye baadhi ya vibanda vidogo vya muda, kama walivyovitengeneza wayahudi kutokana na matawi wakati wa sikuuu ya kiyahudi.

hakujua ambacho alikuwa akisema

Ni kwamba "alikuwa anazungumza bila kuelewa kilichokuwa kinatokea" au, " alizungumza bila kufikiria vizuri kwa sababu alikuwa na furaha sana."

36-05

Sauti toka mawinguni ikisema

Vilevile hii inaweza kutafasiriwa kama, "sauti ilizungumza kutoka mawinguni inasema, "au, Mungu alisikika kutoka mawinguni na kusema."

Msikilizeni Yeye

Hii inaweza kutafasiriwa kama, "ni Yeye pekee ambaye mnapaswa kumsikiliza."

Anguka chini

Huku ni, "kuinama chini kwa haraka" au, "kufika chini ghafla." yaani kusujudu. Hakikisha kwamba tafasiri ya "anguka" haimaanishi ajali. Huenda walifanya hili kwa unyenyekevu na hofu bila kutegemea.

36-06

Aliwagusa

Hii ni "akaweka mkono wake juu yao."Lugha zingine zinaweza kupendelea kuonesha aliwagusa wapi. Kama hivyo, hii ingetafasiriwa kama, "aliwagusa kwenye bega" au, "aliweka mkono wake kwa kila mtu begani."

Msiogope

Hii pia ingelitafasiriwa kwamba, "acha kuogopa"

Inuka

Hii inaweza kutafasiriwa kwamba, "inuka" au, "Tafadhali nakuomba inuka." Hakikisha inaleta maana kwamba Yesu alisema hili kwa upole.

Yesu pekee ndiye alibakia pale

Pia inawezekana kuongeza, Musa na Eliya tayari walishaondoka" yaani hawakuwepo pale.