Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

35-01

siku moja

Hii aya inatambulisha tukio ambalo lilitokea kipindi cha nyuma, lakini haisemi muda kamili. lugha nyingi zina namna moja ya kuanza kutoa habari ya kweli.

Watoza Ushuru

Watoza ushuru walidhaniwa kuwa wenye dhambi kabisa waliiba pesa kwa watuykwa kukusanya ushuru kwa hali ya juu kuliko walivyoagizwa na serikali.

35-02

habari

Yesu alitumia habari hii ili kufundisha ukweli kuhusu ufalme wa Mungu. haiko wazi kama tukio lilitokea kweli au hakuna. kama lugha yako ina habari kama hiyo ya kufikirika au kweli, unaweza kuitumia hapa.

35-03

Urithi wangu

hii ingetafsiriwa kama, "Sehemu ya mali yako ambayo itakuwa haki yangu ya halali unapokufa"

Mali

Hii ni "Mali" au, "milki." Hii mali inaweza pia kuwa ardhi, wanyama, na pesa"

35-04

Alitapanya pesa zake

hiyo ni, "kutumia pesa bila kupata chochote cha thamani kwa kubadilisha." Kwa lugha zingine inaweza kutafsiriwa kama, "Kutupa pesa" au, "Kula pesa zote."

Maisha ya dhambi

hii ni, "kutenda vitu viovu."

35-05

Njaa kali ilitokea

Hii ni, "kulikuwa na chakula kidogo." kwa lugha zingine hii inaweza kutafsiriwa kama, "Kulikuwa na njaa kali."

hakuna pesa kununua chakula

kwa sababu ya njaa, chakula kilikuwa na gharama kubwa, na tayari alishatumia pesa zake zote.

kazi

hii inalenga kazi ambayo unaweza ukafanya kwa ajili ya mtu mwingine ili akulipe pesa. kama hii haiko wazi, hii sentensi inaweza kuanza hivi, "Ili kujipatia pesa, alipata kazi."

Kulisha nguruwe

Hii ni, "kutoa chakula kwa nguruwe." hii pia inaweza kudhaniwa kuwa ni kazi ya hali ya chini katika jamii kwa kipindi hiki. kama lugha yako ina badhi ya maneno kwa kazi ya hali ya chini, tumia neno hili.

35-06

Nafanya nini?

Hii ni, "kwa nini ninaishi hivi?" au, "sipaswi kuishi hivi!" au, "haileti maana kwangu kuishi namna hii." kijana alikuwa haulizi maswali, kwa hiyo lugha zingine zinaweza kutafsiri hii kama maelezo.

35-07

akiwa mbali

hii inaweza pia kutafsiriwa kama, "Ndani ya maeneo ya nyumba ya babaye, lakini bado ni mbali kidogo." kijana alipokuwa akikaribia kwenye nyumba ya baba yake, lakini alikuwa mbali na hata watu wa nyumbani hawakuweza kumwona. Hakikisha isije ikajulikana kuwa alikuwa bado katika nchi tofauti.

akuhurumia

Hii ni, "Alipenda kwa upendo wa dhati na huruma"

35-08

nimekosa mbele za Mungu na mbele zako

hii inaweza kutafsiriwa kama, "Kuasi kinyume na Mungu, na pia nimeasi mbele zako."

Sisitahili

inawezekana pia kusema, kwa hiyo sisitahili" au, "kama matokeo, sisitahili."

35-09

Ndama mzuri

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "Ndama mnene." huyu alikuwa ndama aliyenenepeshwa ili kwamba akipikwa alete radha nzuri.

Mwanangu alikuwa amekufa, lakini sasa ni mzima!

hii ni, "Hii ni kama mwanangu alikuwa amekufa na sasa ni mzima!" au, "niliomboleza kana kwamba " Mwanangu alikufa, na sasa nafurahi kwa sababu ni kama amerudi kuwa hai tena! Baba alitumia maelezo haya ili kueleza furaha aliyonayo kuwa mtoto wake amerudi nyumbani.

alikuwa amepotea na sasa amepatikana

hiyo ni, " ni kama nilikuwa nimempoteza lakini sasa nimepata."

35-10

Muda mfupi

hii inaweza kutafsiriwa kama, "muda si muda" au, "Baada ya muda kitambo."

35-12

Mbuzi mmoja mdogo

Mbuzi mdogo anaweza kuliwa na watu wachache kuliko ndama aliyenona, na asingeweza kuthaminiwa sana. kaka mkubwa analalamika kuwa baba yake anamwona mtoto mwenye dhambi ni mhimu kuliko yeye.

Mtoto huyu ni wako

fafanuzi hii inaonyesha kuwa mtoto mkubwa alikuwa na hasira. inaonyesha kumkataa mdogo wake na kumkasirikia baba yake kwa kumkaribisha nyumbani tena mtoto mpotevu. lugha zingine pia zina njia ambayo si ya moja kwa moja ya mawasiliano ya vitu hivi.

kutumia pesa zako

hii ni, "aliponda pesa ulizompa" au, "alikula mali yako" kama inawezekana tumia maelezo ambayo yanaonyesha hasira za kaka mkubwa.

kuchinja ndama aliyenona

Hii ni, "Kuua ndama aliyenona kwa ajili ya kukla kwenye sikukuu."

35-13

ni haki kwetu

Hii ni, "Ni kitu sahihi kwetu kufanya" au, "Ni kitu sahihi kwetu"

Ndugu yako

baba alirejea kwa mwana wake mdogo kama, "Ndugu yako" kumkumbusha mwana mkubwa mahusiano yake kwa mdogo wake na alivyopaswa kumpenda mdogo wake.

alikuwa amekufa, lakini sasa yuko hai

Angalia jinsi unaweza kutafsili hii

alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana!

Angalia jinsi unaweza kutafsili hii