Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

04-01

Miaka mingi baada ya gharika

Vizazi vingi vimepita baada ya gharika

tena, watu wengi

Familia ya Noah iliongezeka na kuwa na watu wengi wa kuujaza mji

lugha inayofanana

Hii inamaanisha kulikuwa na lugha mojja hivyo watu walielewana

mji

Ni vyema kutumia neno la jumla linalomaanisha mji kwakuwa kifungu hakitaji jina maalumu.

04-02

mnara mrefu kuifikia mbingu

mnara huo ulikuwa mrefu kiasi kwamba ncha yake ilifika angani.

Mbingu

Hii inaweza pia kutafsiriwa kama "anga."

04-03

alibadili lugha yao

Kwa ghafla Mungu aliwapa lugha tofauti tofauti na hivyo hawakuweza kuelewana tena.

lugha nyingi mbalimbali

Badala ya kundi moja kubwa kuzungumza lugha moja, sasa waligawaanyika katika makundi mengi madogo madogo na kila kundi likawa na lugha yake.

aliwatawanya watu

Wakati Mungu alipobadilisha lugha zao, alisababisha watu hao kutawanyika na kila kundi lilienda sehemu yake.

Babeli

Hatujui kwa hakika mahali ambapo mji huu ulikuwa, zaidi ya kwamba ulikuwa mahali fulani huko Mashariki ya kati.

alichanganya

Hii inaelezea jinsi ambavyo watu walichanganywa wakati ambapo hawakuweza kuelewana baada ya Mungu kubadili lugha yao.

04-04

Mamia ya miaka baadaye

Hii inaweza kutafasiriwa kama, "vizazi vingi baada ya watu kugawanyika katika lugha mbalimbali."

Ondoka katika nchi yako

Hii inaelezea eneo ambalo Abramu alizaliwa na kuishi.

na familia yako

Mungu alikuwa anamwita Abramu na famia yake tu, na kuwaacha ndugu zake wengine.

kukufanya kuwa taifa kubwa

Mungu angemfanya Abramu kuwa na watoto wengi, na wangekuwa taifa kubwa na la muhimu.

04-05

alichukua

lugha zingine zinaweza kusema "alileta"

Mungu alimuonesha

kwa namna fulani Mungu alimudokezea Abramu kuhusu mahali alipopaswa kwenda. Kifungu hiki hakielezi jinsi ambavyo Mungu alimuonesha.

nchi ya Kanaani

jina la nchi hiyo iliitwa "Kanaani."

04-06

ardhi yote utakayoiona

Kama Abramu alikuwa amesimama juu mlimani, angeweza kuona eneo kubwa.

kama urithi

Mungu aliahidi kumpa Abramu na uzao wake ardhi kama vile baba huwa watoto wake ardhi mali.

Kisha Abramu akakaa katika nchi

Abramu aliishi mahali pale pamoja na wote alioenda nao.

04-07

Melkizedeki

Melikizedeki alikuwa ni mtu mwenye mamlaka ya dini katika Kanaani ambaye alipokea sadaka na kuziwasilisha kwa Mungu.

Mungu aliye juu

Watu wa Kanaani waliabudu miungu mimgi ya uongo. Jina "Mungu aliye juu" lilimtambulisha Mungu wa kweli ambaye Melkizedeki alimwabudu.

04-08

Miaka mingi

Miaka mingi ilipita tangu Mungu alipomuahidi Abramu mtoto.

kama nyota angani

msemo huu unamaanisha kuwa uzao wa Abramu utakuwa na watu wengi kiasi kwamba hakuna atakayeweza kuwahesabu.

04-09

pande mbili

sehemu hizi mbili zinaweza kuwa, watu wawili, makundi mawili ya watu, au mtu mmoja na kundi la watu. Katika hili patano lilikuwa kati ya Mungu na Abramu.

kutokana na mwili wako

Kwa mwili wake binafsi Abramu angempa mimba mkewe, ili kwa pamoja wapate mtoto wao kwa njia ya asili. Hii ilikuwa ni ahadi ya ajabu sana maana Abramu na sara walikuwa wazee sana.

Hawakuwa na mtoto wa kiume

Abramu hakuwa na uzao ambao wangeirithi ardhi yake.