Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

37-01

Siku moja

Maneno haya yanaonesha tukio lililotukia kipindi kilichopita, lakini hayaelezi muda maalumu. Lugha nyingi zinanjia inayofanana katika kuanza kusimulia habari ya kweli.

Mariamu

Mama yake Yesu pia aliitwa Mariamu. Huyu alikuwa ni mwanamke mwingine tofauti na mama yake Yesu.

Ugonjwa huu siyo wa kifo

Hii inaweza kutafsirika kwamba, "matokeo ya ugonjwa huu siyo kifo" au, Lazaro ni mgonjwa, lakini kifo hayatakuwa matokeo kwenye ugonjwa huu." Huenda wanafunzi wa Yesu walifikiri inamaanisha kwamba Lazaro asingelikufa. Lakini Yesu alijua kwamba, ingawaje Lazaro atakufa kutokana na ugonjwa wake mwisho wake atakuwa hai.

Ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu

Hii ni, "hii itawasababisha watu kumtukuza Mungu kwa jinsi alivyo mkuu."

Lakini alisubiri mahali alipokuwa kwa siku mbili

Hii ingelitafasiriwa kuwa, "lakini alibaki mahali alipokuwa kwa siku mbili, hata kama walitaka aende na amponye Lazaro.

37-02

Uyahudi

Hii inarejea sehemu ya kusini mwa Israeli, ambako waliishi kabila la Yuda. Lugha nyingine itapendelea kusema, "mkoa wa uyahudi."

Amelala usingizi, na lazima nimwamshe

Tafasiri kipengele hiki kwa maneno ya kawaida kwenye lugha yako yaani "kulala" na "amka." Ingawa Yesu alikuwa akitumia maneno haya akiwa na maana nyingine, bado wanafunzi hawakumwelewa.

37-03

Atapata nafuu

Wanafunzi walidhani, "hakuna sababu ya sisi kwenda kwake sasa, sababu atapata nafuu."

Nafurahi

Inaweza kutafasiriwa kuwa, "mimi ninafuraha" au, "hiyo ni nzuri." haina maana alikuwa na alifurahia kifo cha Lazaro, lakini zaidi kwamba alikuwa na furaha kwamba Mungu alikuwa aoneshe jinsi alivyo mkuu.

37-04

Martha

Martha alikuwa dada wa Lazaro na Mariamu.

Alikwenda kukutana na Yesu

Hii ni kwamba, "alikwenda kumwona Yesu alipokuwa anakuja mjini."

Kaka yangu asingelikufa.

Hii ni, "ungelimponya kaka yangu na asingelikufa" au, "ungelizuia kufa kwa kaka yangu."

Lolote uombalo toka kwake atakupa

Hii ni, "atanfanya lolote unalomwomba toka kwake."

37-05

Mimi ni ufufuo na uzima

Hii, "mimi" iliyotumika hapa ni kauli mojawapo yenye nguvu sana kati ya kauli zake Yesu anazosema kuhusu uasili wake. Hapa Yesu anaashiria kwamba yeye ni "mpaji" au "chanzo" cha ufufuo na uzima. Ikiwezekana tafasiri maneno haya kwa namna ambayo inaweka wazi umhimu wa asili. Hii inaweza kutafasirika kwamba, "Mimi ndiye hufufua watu na huwapa uzima"

Ataishi hata kama akifa

Hii ni, "hata kama atakufa, ataishi milele." Neno la kiingereza "Yeye" si kwamba linarejea kwa wanaume tu pia wanawake wanaoamini wataishi milele.

Martha

Martha alikuwa dada yake Lazaro na Mariamu.

Hatakufa

Hii inaweza kutafasiriwa kwamba, "ataishi milele."

37-06

Mariamu

Huyu ni mwanamke ambaye siyo mama yake Yesu.

Alianguka miguuni pa Yesu

Hii ni, "alipiga magoti miguuni pa Yesu" ikiwa ishara ya heshima.

Kaka yangu hangelikufa

Ni kwamba, "ungelifanya kaka yangu asife" au, "ungalizuia kifo cha kaka yangu" au, "kaka yangu angelikuwa hai."

37-07

Yeye aliwaambia

Hii ni, "Aliwaambia watu pale." Huenda alikuwa hawaambii Martha na Mariamu kuliondoa jiwe.

Ondoa jiwe

Baadhi ya lugha zitapendelea kusema, "ondoa jiwe kutoka kwenye kaburi."

Martha

Martha alikuwa dada yake Lazaro na Mariamu.

Amekufa kwa siku nne

Hii pia inatafsirika kama, "Alikufa siku nne zilizopita na mwili wake umelazwa pale."

37-08

Mimi sikuwaambia ninyi?

Hili, "kumbukeni kwamba niliwaambia." Si kwamba Yesu anawauliza swali ili apate jibu, hivyo lugha zingine zitatafsiri hii kama amri.

Ona utukufu wa Mungu

Hii ni, "tazama utukufu wa Mungu uliyodhihilishwa" au "tazama Mungu anavyoonesha ukuu wake."

Liondoe jiwe

Baadhi ya lugha zitasema, "liondoeni jiwe mahali pa mlango wa kaburi."

37-09

Unanisikia

Hii ni, ""unanisikiliza." Inaweza kusaidia kuongoza, "kama niombavyo kwako" au, "nizungumzapo kwako."

Njoo nje

Baadhi ya lugha zinaweza kupendelea kusema, "toka nje kaburini"

37-10

Lazaro alikuja kutoka nje

Baadhi ya lugha zitasema, "Lazaro toka kaburini."

Sanda

Hii ni, "nguo za kuzikia" Hii inawea kutafsirika kama, "sanda" au, "vazi maalumu."

Sababu ya muujiza huu

Hii ni, "kwasababu Mungu alishafanya muujiza huu wa kushangaza" au, "kwasababu Yesu tayari alishamfufua Lazaro."

37-11

Wivu

Huo ni "wivu wa Yesu wa nguvu na mashuhuri " au "wivu ambao wayahudi walikuwa wanauamini kwa Yesu."

Kusanyika pamoja

Hiyo ni, "kutana pamoja" au, "unganisha pamoja." huu haukuwa mkutano wa kawaida, lakini ni mkutano maalumu kwa lengo la kupanga jinsi ya kumuua Yesu.