Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

26-01

Baada ya kushinda majaribu ya shetani, Yesu alirudi

Unaweza kuliweka jambo hili katika sentensi mbili na kusema, " Yesu hakufanya mambo mabaya ambayo shetani alijaribu kumshawishi kufanya na kwa hiyo alimshinda. Na baada ya hayo, Yesu alirudi." Neno "kushinda" linaweza pia kutafasiriwa kwa " Kupinga" au "Kukataa" au "Kutokubali"

Katika Nguvu ya Roho Mtakatifu

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "Wakati nguvu ya Roho Mtakatifu ikifanya kazi ndani yake" au " Na Roho Mtakatifu alikuwa akimwongoza kwa nguvu."

Alikwenda kila mahali akifundisha

Hii ni kwamba, "Alisafiri kwenda miji tofauti na sehemu zingine na akafundisha watu pale."

Kila mmoja

Hii ni kwamba, "Kila mmoja aliye mjua au kusikia habari zake."

Alimsema vizuri

Hii ni kwamba, "Alisma mambo mema juu yake."

26-02

Mahali pa ibada

Hii ni, "Jengo ambalo wayahudi walikusanyika kumwabudu Mungu." Hii pia inaweza kutafsiriwa kama jengo la ibada."

Gombo

Gombo lilikuwa ni karatasi ndefu au ngozi ambayo ilikunjwa ambayo ilikuwa na maandishi juu yake.

Gombo la nabii Isaya

Hii ni, " Gombo ambalo lilikuwa na maneno ambayo nabii Isaya alikuwa ameandika." Isaya alikuwa ameandika juu ya gombo mamia ya miaka kabla. Hii ilikuwa ni nakala ya gombo hilo.

Alifungua gombo

Hii inaweza kutafsiliwa kama, "Alifungua gombo" au, "Alilikunjua gombo.

26-03

Tangaza habari njema kwa masikini

Hii ni, "Waambie masikini na wahitaji habari njema kwamba Mungu atawasaidia."

Uhuru wa ufungwa

Hii ni, Kuwaambia watu ambao ni wakosaji kifungoni kwamba wataachiliwa."

26-04

Maneno niliyosoma mbele yenu yanatokea sasa

Njia zingine za kutafsiri hii zingekuwa, "Maneno ambayo umeyasikia nikiyasoma yametimilika sasa" au "Leo maneno niliyoyasoma kwenu yametimi kama mlivyoyasikia."

26-05

hakuna nabii anayekubalika katika mji wa kwao

Sentensi hii inamaana, "watu hawatambuwi mamlaka ya nabii aliyekulia katikati yao."

26-06

Elisha

Elisha alikuwa nabii wa Mungu ambaye alikuja baada ya Eliya. Kama vile Eliya, Elisha aliwakabili wafalme wa waisrael ambao walifanya dhambi dhidi ya Munguna alifanya miujiza ambayo Mungu alimpa uwezo wa kuifanya.

kamanda

Huyu ni "kiongozi wa jeshi."

wakawa na hasira juu yake.

Wayahudi hawakupenda kusikia kuwa Mungu amebariki kundi la watu wowote isipokuwa waowenyewe, kwahiyo wakawa na hasira kwa kile ambacho Yesu alifanya.

26-07

mahali pa kuabudia

Hii ni, "nyumba ambayo wayahudi walikusanyika kumwabudu Mungu." hii pia inaweza kutafsiriwa kama " Nyumba ya ibada."

Lakini Yesu akaondoka Mbele yao

"Lakini" inaweza kutafsiriwa kwa neno zito la kukanusha au sentensi kam vile "Lakini badala yake" au, "Hatahivyo" kuonesha kwamba watu hawakuweza kufanya lolote walilolipanga kumfanyia Yesu.

26-08

alienda mpaka mkoa wa Galilaya

Hii ni kwamba, "Sehemu zote katika galilaya" au, kutoka mali hadi mahali pengine katika Galilaya

26-09

waliokuwa na mapepo ndani yao

Hii ni, "ambao walitawaliwa na roho za kiovu."

Yesu alipo waamuru.

Hii inaweza pia kutafsiriwa kama, " wakati Yesu aipotoa amri kwao."

26-10

walijifunza kutoka kwake.

Hii ni kwamba, "walijifunza kutoka katika yale aliyowafundisha" au, "walijifunza katika yote aliyosema na kutenda."