Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

40-01

walimpeleka

Hii ni, " walimlazimisha kwenda naye." Hii inaweza pia kutafsiriwa kama, "walimchukua."

Kumsulibisha

Hii ni, "Kumuua juu ya msalaba."

40-02

Fuvu

Mlima uliokaribu na Yerusalemambao una mawe meupe juu yaliyo mithili ya sehemu ya juu ya fuvu.

Wasamehe, kwa sababu hawajui watendalo

Hii ni, "Hawajui maana ya jambo ambalo wanalifanya, kwa hiyo tafadhali wasamehe." Maaskari walidhani kuwa Yesu alikuwa mharifu aliyestahili kufa. Hawakuelewa kuwa alikuwa mwana wa Mungu.

40-03

Wlipigia kura mavazi ya Yesu

Hii inamaana, "walifanya mchezo wa bahati ya kushinda nafasi ya kuchukua mavazi ya Yesu." Hatujui jinsi gani walifanya haya, lakini katika baadhi ya tamaduni indeweza kutafsiriwa kama, "kutupa mawe kwenye ardhi kwa ajili ya kujishindia mavazi ya Yesu" au, "Kuchagua vijiti ili kuamua nani angeweza kushinda kuchukua mavazi ya Yesu."

Walitimiliza unabii amabao ulisema

Hii ni, "Walifanya kile ambacho maandiko yalitabiri muda mrefu uliopita kuhusu jambo ambalo lingetokea kwa Masihi." au, "Walifanya jambo ambalo nabii aliandika muda mrefu uliopita."

40-04

Wanyang'anyi wawili

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "majambazi wawili" hawa ni watu ambao ni wahalifu ambao walitumia nguvu kuiba vitu.

Je huna hofu ya Mungu?

Mwizi hategemei jibu la swali hili, ni njia ambayo baadhi ya lugha hutumia kuweka sentensi yenye mkazo. kama lugha yako haitumii maswali kama ilivyo hapa, hivyo tafsiri jambo hili kama, "Lazima uwe na hofu ya Mugu!"

Sisi tunahatia lakini mtu huyu hana hatia

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "wewe na mimi tumefanya mambo maovu na tunastahili kufa, lakinimtu huyu, Yesu, hajafanya kitu chochote kibaya na hastahii kufa," "sisi" neno hili linajumuisha wezi, lakini halijumuishi Yesu.

Mtu huyu

Sentesi hii inamaanisha Yesu.

Tafadhali unikumbuke

Hii inamaana, "Tafadhari nipokee" au, Tafadhali nikaribishe" au, "niruhusu niwe pamoja na wewe." "Kumbuka" mahali hapa halimaanishi kukumbuka jambo baada ya kulisahau. Tafsiri jambo hili katika njia ambayo itawasilisha ombi la kumsihi mtu.

Katika ufalme wako

Hii ni, Wakati utakapo simamisha ufalme wako" au, "wakati unatawala kama mfalme."

Paradiso

Hili ni jina lingine la "Mbinguni"

40-05

Tutakuamini

Hii ni, "Tutakuamini" au, " Tutaamini kuwa wewe ni Masihi."

40-07

Imekwisha

Hii inaweza pia kutafsiriwa kama, "imekwisha" au, imemalizika" au, "Nimeimaliza" au, "nimemaliza kazi." Hii inamaana kazi ya Yesu ya wokovu ilikuwa imemalizika.

Mikonono mwako

Hii inamaana, "chini ya uangalizi wako"

Akainamisha kichwa

Hii inamaana aliinama kichwa chake."

Akaitoa roho yake

Hii ni, " aliitoa roho yake kwa Mungu" au, "aliikabidhi roho yake kwa Mungu na akafa."

Pazia kubwa

Hii ilikuwa nguo ya kitambaa kubwa, imara imening'inizwa hekaluni. Ilikuwa kama ukuta uliotenganisha chumba kimoja na kingine. Inaweza pia kutafsiriwa kama, pazia nene" au, "nguo ya kitambaa iliyo ning'inizwa" au, " chandarua , ngao."

40-08

Kupitia kifo chake

Hii ni, "Kwa njia ya kifo chake" au, "kwa kufa kwake."

Alifungua njia

Hii ni, " alifanya iwezekane."

Kuja kwa Mungu

Hii ni, " kuja karibu na Mungu" au, " nenda karibu na Mungu" au, "karibia Mungu" au, "kumjua Mungu ki- binafsi." Kuchanika kwa pazia kulionesha kwamba kizuizi kati ya Mungu na watu kimeondolewa.

40-09

Yusufu

Huyu hakuwa ni mume wa Mariam. Alikuwa ni mtu mwingine aliye itwa Yusufu.

Alimuomba Pilato auchukuwe mwili wa Yesu

Hii ni kwamba, "alimuomba Pilato awaruhusu kuuchukua mwili wa Yesu kutoka msalabani."