Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

28-01

Sikumoja

Sentensi hii inatoa utangulizi wa jambao ambalo lilitokea nyakati za nyuma, lakini halielezi muda maalumu. Lugha nyingi zina namja hii ya kuanza kueleza simulizi ya kweli.

Kiongozi kijana tajiri

Huyu kijana alikuwa tayari ni tajiri na kiongozi mwanasiasa mwenye nguvu, ingawa alikuwa bado ni kijana.

Alimwendea Yesu

Hii ni kwamba alimfuata Yesu

Mwalimu Mwema

Hii inamaanisha "Mwalimu mwenye haki" Alikuwa hamaanishi kuwa Yesu alikuwa tu ni mwalimu aliye pitia mafunzo.

Kuwa na uzima wa milele

Hii ni kwamba, "Kupokea uzima wa milele" au. "Kuishi na Mungu milele na milele."

Kwa nini kuniita "mwema"

Yesu hakatai kuwa yeye ni Mungu, isipokuwa anamuomba mtawala kuelewa kuwa Yesu ni Mungu.

Kuna mmoja tu aliye mwema, na huyo ni Mungu

Njia nyingine ya kusema hili ingelikuwa, "Aliye mwema kweli kweli ni mmoja tu ambaye ni Mungu." au, "Mungu ndiy pekee aliye mwema kweli kweli."

28-02

Ni mambo gani nahitaji kutii?

Hii ni kwamba, "Ni sheria gani zitakazo tosheleza mimi kupokea uzima wa milele?"

Kama unavyo jipenda mwenyewe

Hii ni kwamba, "kadiri unavyo jipenda mwenyewe" au, "kiwango kile kile unacho jipenda mwenyewe,"

28-03

Tangu nikiwa kijana

Njia nyingine ya kusema hili ingekuwa, "kuanzia wakati nilipo kuwa mtoto hadi sasa."

Jambo gani ambalo bado napaswa kulifanya?

Hii ni kwamba, "Nini zaidiambacho nahitajika kukifanya" au, Nahitaji kufanya nini kama nyongeza ya haya niliyokwisha fanya?"

Akampenda

Yesu alimuhurumia. chagua nenolinalo maanisha upendo ambao unalingana na ule upendo ambao Mungu anao kwa watu.

28-04

Wewe

Kama lugha yako ina neno tofauti na "wewe"kutegemeana na idadi ya watu waliokusudiwa, tumia hali ya umoja.Yesu alikuwa anasema amri hii kwa mtu huyu mmoja.

Mkamilifu

Hii inamaana, "mtu wa haki kabisa."

Kila kitu unachomiliki

Hii ina maana, "kilakitu ambacho ni mali yako."

Hazina

Hii pia inaweza kutafsiriwa kama, "utajiri" au, utajiri mwingi"

Mbinguni

Hii inaweza kutafsiriwa kuwa, " iliyo mbinguni wakati utakapofika pale," kinyume na utajiri ambao Yesu alimwambia kijana kuutoa "hapa na sasa."

28-05

Aliposikia alicho kisema Yesu

Hii ni kwamba, aliposikia Yesu akimwambia kutoa alivyo kuwa navyo."

28-06

Kuingia katika ufalme wa Mungu

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "kufanyika raia katika ufalme wa Mungu."

Ngamia

Ngamia ni wanyama wakubwa ambao maranyingi wanatumika kubeba mizigo mizito. ikiwa ngamia hawajulikani katika lugha ya eneo lako,sentensi kama,"Myama mkubwa sana" au, Mnyama wa mzigo" linaweza kutumika. ikiwa utachgua kutumia mnyama mkubwa badala ya ngami, hakikisha kuwa mnyama unaye mtumia anajulikana na watu kama vile watu ambao Yesu alizungumza nao walivyo mjua mnyama. kama vile , "Punda."

Tundu la sindano

Hii inarejea kwenye tundu dogo mwishoni mwa sindano ya kushonea nguo. Wazo la kitu kikubwa kama ngamia kupita katika tundu la sindano imekusudiwa kuwakilisha jambo ambalo haliwezekani.

28-07

Shikwa na mshangao

Hii ni hali ya, "kustajabisha

Nani anaweza kuokoka

Hii pia inaweza kutafsiriwa kama, "ikiwa watu matajiri hawezi kuokoka, nji jinsi gani mtu wingine yeyote anaweza kuokoka?" Watu wengi waliamini kuwa kuwa tajiri ni dalili ya kupata upendeleo wa Mungu.

Okoka

Hapa inarejea katika hali ya kuokoka katika hukumu ya Mungu na hukumu ya dhambi na kuruhusiwa kuwa raia katika ufalme wa Mungu.

28-08

"Kwa watu mambo haya hayawezekani

Hii ni kwamba, haiwezekani kwa watu kufanya hivi" au, watu wenyewe hawawezi kujiokoa wenyewe."

kwa Mungu mambo yote yanawezekana".

Hii inaweza pia kutafsiriwa kama, "Mungu anaweza kufanya jambo lolote, hata kuokoa mtu tajiri" au, Mungu anaweza kufanya mambo yasiyowezekana, kwa hiyo anaweza kuokoa hata mtu tajiri."

28-09

Tumeacha kila kitu

Hii ni kwamba, kuachana na mambo yote" , au, kuachilia vitu vyote tulivyo miliki."

Je, tutapata thawabu gani?"

Njia nyingine ya kusema hivi ni, " ni zawadi gani tutapokea" au, Ni jinsigani tutazawadiwa?" inaweza pia kuwa muhimu kuongeza, kwa sababu tumefanya hivi?"

28-10

Aliye acha

Hii ni mtu "aliye acha" au, " aliye achana " au,"aliye hesabu jambo kutokuwa la muhimu kuliko Mungu.

Kwa ajili yangu

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "Kwa sababu yangu" au, kwa ajili yangu."

Mara 100 zaidi

Hii inamaana, "zaidi sana kuliko alivyo kuwa navyo mwanzoni."

Wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho

Hii ni, " watu ambao ni wa muhimu sasa, hawata kuwa wa muhimu baadaye."

Wengi wa mwisho watakuwa wa kwanza

Hii ni kwamba, wale wanaofikiriwa kuwa si wa muhimu duniani watafikiriwa kuwa wa muhimu mbinguni" au, "watu wengi ambao wanadhaniwa sasa kuwa na thamani ndogo hapa duniani watathaminiwa zaidi mbinguni."