03-01
baada ya muda mrefu
Simulizi hii ilitokea baada ya vizazi vingi (mamia ya miaka) baada ya uumbaji.
walikuwa waovu na katili
Ni rahisi kusema, "walikuwa waovu na walifanya mambo ya ukatili."
ikawa mbaya
Inaweza kueleweka kwa kusema "Watu walikuwa wakiishi kwa njia ya uovu na ubaya ambazo hazikumpendeza Mungu."
Mungu aliamua kuwaangamiza
Hii haimaanishi kuwa dunia itaharibiwa kabisa. ila Mungu alikusudia kuwaangamiza watu wote waliomuasi Yeye na walio sababisha maovu na ukatili. Mafuriko pia itauwa wanyama na ndege wote katika nchi.
Mafuriko makubwa
Maji mengi ambayo yengeifunika dunia, hata sehemu ambazo mara nyingi ardhi i kavu, na hata kufunika vilele vya milima mirefu.
03-02
akapata kibali
Mungu alipendezwa na Nuhu, kwasababu alimcha na kumtii Mungu. Japokuwa siyo kwamba Nuhu hakuwa na dhambi, Mungu alimhurumia na akaweka mpango wa kumuokoa yeye na familia yake kutoka kwenye mafuriko makubwa. Hakikisha haitaonekana kana kwamba Nuhu alipata bahati, au kwamba ilitokea tu akaponyoka. Bali, ni mpango na chaguo la Mungu.
Mafuriko
Maji mengi yenye kuleta maafa.
mpango wa kutuma
Mungu alipanga kuleta mafuriko yatakayo funika dunia mzima kwa kuruhusu mvua nyingi. Hii ni kwamba alipanga kusababisha mafuriko ya mvua nyingi.
03-03
safina
Safina ni aina ya mashua ambayo ni kubwa kiasi kwamba inaweza kubeba watu wanane, na wanyama wawili wawili kwa kila kundi la wanyama, pamoja na malisho yao kwa kadri ya muda wa mwaka mmoja.
03-04
Nuhu aliwaonya
Nuhu aliwaambia watu wote kuwa Mungu ataiangamiza dunia kwa sababu ya dhambi.
wamrudie Mungu
Hii ilimaanisha kuacha kufanya dhambi na kuanza kumtii Mungu.
03-06
Mungu akatuma
Muhu alikuwa hana haja ya kuwatafuat wanyama bali Mungu aliwatuma kwake.
waliotumika kwa sadaka ya kuteketezwa
Kwa lugha nyingie, inaweza kuwa rahisi kusema kuwa "wanyama wale waliokubalika na Mungu kwa sadaka ya kuteketezwa." Mungu aliamua watu wamtolee wanyama kama sadaka ya kuteketezwa, hata hivyo aliwaruhusu tu Kumtolea aina fulani ya wanyama.
Mungu mwenyewe alifunga mlango
Hii inatia mkazo kuwa ni Mungu mwenyewe ndiye aliyefunga mlango.
03-07
mvua iakaanza kunyesha, na kunyesha , na kunyesha
Hii inasisitiza kuwa kulikuwa na mvua isyokuwa ya kawaida, mvua kubwa sana. Lugha nyingine huenda zina namna ya kutia mkazo.
maji pia yalitokea ardhini
Hii iliashiria kulikuwa na maji mengi yaliyotokea ardhini.
Dunia yote ikafunikwa
Hii ilimaanisha dunia yote ilifunikwa na maji.
03-09
Mvua kukatika
Hii inaweza kutafsiriwa kuwa, "mvua iliacha kunyesha."
Safina ikatua
Kulikuwepo na maji mengi kutokana na mvua iliyofunika hata milima. Safina ilielea mlimani na maji yalipoanza kwenda chini, safina ilienda chini na maji na safina ikatulia kwenye mlima.
miezi mitatu baadaye
Maji yaliendelea kupungua kwa muda wa miezi mitatu baadaye.
milima ilionekana
Njia nyingine za kutafsiri hii ni "vilionekana" "vikatokeza", vilikuwa vimeonekana. "Inaweza ikawa rahisi kusema, "Baada ya miezi mitatu, maji yalishuka kiasi kwamba Nuhu na familia yake walianza kuona vilele vya milima.
03-10
kunguru
Aina ya ndege mweusi anayeruka na kula aina ya majani na wanyama, ikiwa ni pamoja na nyama zilizooza za wanyama.
03-11
njiwa
Ndege mdogo mweupe na kijivu mwenye kuruka na kula mbegu na matunda.
tawi la mzabibu
Mti wa mzabibu una mafuta ambayo watu hutumia kupikia na kujipaka. Kama lugha yako haina neno la "tawi la mzabibu" unaweza kutafsiri kama ni tawi linalotokana na mti uitwao "mzabibu" au tawi kutoka kwa "mti wenye mafuta."
maji yalianza kukauka/kwenda chini
Inaweza ikawa rahisi kwa lugha yako kusema, maji yaliendelea kuisha, au "kiwango cha maji kilipungua au kilishuka."
03-12
alisubiri wiki moja zaidi
Unaweza kusema, alisubiri suku zaidi, Neno "kusubiri" inaonyesha kuwa Nuhu alisubiri ili maji yakauke kabla ya kumtuma njiwa tena.
03-13
Miezi miwili baadaye
Hii ina maana miezi miwili baada ya Nuhu kumuachia njiwa kutoka katika safina. Huenda ni muhimu kusema hii kwa lugha rahisi kama haijaeleweka.
Muwe na watoto wengi
Hakikisha inaeleweka kuwa ni amri na shauku ya Mungu, unaweza kusema "Ni lazima kuwa na watoto wengi" au "Nataka ninyi muwe na watoto wengi."
Muijaze nchi
Kama haijaeleweka, unaweza ukasema "muijaze dunia na watu" au "ili pawepo na watu wengi waishio duniani."
03-14
aina ya wanyama waliopaswa kutolewa dhabihu
Njia nyingine ya kusema hii ni, "wanyama ambao watu hutumia kumtolea Mungu dhabihu ya kuteketezwa."
Mungu alifurahishwa
Mungu alipendezwa na Nuhu kwa kumtolea dhabihu ya kuteketezwa kwa wanyama hao.
03-15
kamwe tena
Hii inamaana "hatarudia tena" au "hatarudia tena wakati wowote" mifano: "Sitalaani tena ardhi" au sitalaani tena ardhi kwa wakati wowote au kwa hakika sitalaani tena ardhi.
kulaani ardhi
Ardhi na viumbe vingine vyote hutaabika kwa sababu ya dhambi za wanadamu.
Dunia
Hii inamaanisha ardhi na viumbe vingine vyote vinavyoishi duniani.
watu ni wenye dhambi tangu utotoni mwao
Njia nyingine ya kusema hii ni, "watu hufanya matendo maouvu kwa maisha yao yote."
03-16
upinde wa mvua
Huu ni upinde wa mwanga wenye rangi ambazo mara nyingi hutokea angani pale panapo kuwepo na mvua ya ngurumo.
ishara
Ishara ni kama kitu au tukio ambayo ina maana fulani au inayoashiria kitu ambacho ni cha kweli au kitatokea.
ishara ya ahadi yake
Kwa lugha nyingine inaweza ikawa vizuri kusema "kuonyesha kuwa ameahidi."
kila wakati
Hakikisha inafahamika ya kuwa, ni kila wakati upinde wa mvua inaponekana na kuendelea. Huenda ni Muhimu kuongeza, "Kuanzia sasa na kila wakati."
alicho ahidi
Hii inarejea, ile hali ambayo Mungu aliahidi kutoangamiza dunia tena kwa kutumia mafuriko.