44-01
Siku moja
Hii sentensi inatoa utangulizi wa tukio amabalo limetokea wakati ulio pita, lakini halielezi muda maalumu. lugha nyingi zina usemi wa jinsi hii wakati wa kuanza kueleza simulizi ya kweli.
Mtu aliye kiwete
Hii inaweza pia kutafasiriwa kama, " kilema." Hii inamaanisha mtu ambaye hawezi kutumia miguu yake kwa ukamilifu, na hawezi kusimama au kutembea.
44-02
Katika jina la Yesu
"Jina" hii inasimama badala ya mamlaka na nguvu za mtu. Kwa hiyo usemi huu unamaanisha, " Kwa mamlaka ya Yesu."
Simama
Hii maana yake ni , "simama juu."
44-03
Ua wa hekalu
Ni makuhani pekeyao ndio ambao waliingia hekaluni, lakini wayahudi wa kawaida waliruhusiwa kuja katika eneo hili ambalo lilizunguka hekalu.
44-05
Mwanzilishi wa uzima
Hii ni kwamba, Yule aliye umba uzima" au, "yeye yule atupaye uzima" au, yeye ambaye anafanya watu waishi" hii inamaanisa Yesu.
Matendo yako
Hii pia inaweza kutafsiriwa kama, "mambo uliyofanya." Hii inamaanisha maswali yao juu ya Pilato kumuua Yesu.
Mrudie Mungu
Hii maana yake ni kwamba, "amua kumtii Mungu."
Dhambi zako zitasafishwa
Hii inaweza kutafsiriwa kama, "Mungu ataosha dhambi zenu" au, Mungu ataondoa dhambi zenu ana kuwafanya muwe safi." hii inazungumzia Mungu kuwatakasa watu katika roho zao kwa kuondoa dhambi zao kabisa. Hii haimaanishi tendo halisi la kuosha.
44-06
Ujumbe wa Petro
Hii ni, " ujumbe ambao Petro alikuwa amewahubiri."
Idadi ya wanaume
Hii ilikuwa ni ongezeko la idadi ya wanawake na watoto ambao waliamini
44-08
Kuponywa
Hii maana ya keni , " kuwa salama" au, "kuwa mwenye nguvu"
Walimkataa
Hii ni, " walikataa kumpokea" au, "walikataa kumwamini Yesu" au, walikataa kuamini kuwa Yesu ni mwokozi."
Lakini hakuna njia nyingine ya kutuokoa isipokuwa kupitia uwezo wa Yesu
Hii inaweza kutafsiriwa kama, "Lakini njia pekee ya kuokolewa ni kupitia uwezo wa Yesu Kristo" au, " lakini Yesu pekee anaweza kutuokoa, kwa uwezo wake."
Kuokolewa
Hii inaweza kutafsiriwa kama, "kuokolewa kutoka dhambi zetu" au, "kwamba tunaweza kuokolewa kutoka katika dhambi zetu."
44-09
Walishangazwa
Hii ni kwamba, " walistaajabu" au, walishangaa."
Kawaida
Hii ni ile "iliyozoeleka" ya hali ya chini." Petro na Yohana walikuwa wavuvi wa kawaida.
Ambao hawakuwa na elimu
Hii ni kwamba, "ambao hawakuwa na elimu ya darasani." hii pia inaweza kutafsiriwa kama, "ambao hawajaenda kwenye shule ya dini."
Kisha walikumbuka
Hii inaweza kutafsiriwa kama, " lakini kisha walifikiri juu ya ukweli kwamba."
Walikuwa pamoja na Yesu
Hii inaweza pia kutafsiriwa kama, "walitumia muda pamoja na Yesu" au, walikuwa wamefundishwa na Yesu."
Baada ya kutishwa
Viongozi walisema wangemuadhibu Petro na Yohana kama wangeendelea kuwafundisha watu kuhusuYesu.
Waruhusu waende
Hii ni kwamba, "waliwaruhusu waondoke."