Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

20-01

Walivunja agano

Hii ni kwamba, " hawakuzitii amri za Mungu alizowapa ndani ya agano lake katika Mlima Sinai."

Aliwaonya watubu na wamwabudu yeye tena.

Namna nyingine ya kutafasiri ni, " aliwambia waache kutenda dhambi na wamwabudu Yawee badala ya miungu mingine, au mabaya yatawapata."

20-02

Falme zote

Hii ilimanisha falme zote za Israel na Yuda.

Ufalme

Nchi iliitwa "Ufalme" pale ambapo ilikuwa na nguvu kuongeza mamlaka yake kuzitawala nchi zingine."

Kunyang'anya

Hii ni inamaanisha kuwa, "kuiba". waliiba baadhi ya vitu na wakavibeba kuvipeleka Ashuru.

20-03

Wenye ujuzi

Hii inarejea ujuzi wa vitendo kama vile, fundi wa mbao, mtengeneza vyuma na mjenzi.

Walibakia

Inamaanisha, " walibaki" au " waliachwa" au " waliruhusiwa kubaki"

20-04

Wageni katika nchi isiyokuwa yao.

Hii inarejea watu wasiyokuwa wa israel.( wageni katika nchi ya israel).

20-05

Kwa kutokumuamini na kumtii yeye

Namna nyingine ya kusema ni, "Kwa sababu hawakumuamini na kumtii yeye."

Aliwaonya.

Hii ni kwamba, "Aliwaambia waache kutenda dhambi au mabaya yatawapata.

Walikataa kusikia.

Inamaana ya kuwa, "walikataa kutii" au "walikataa kuziacha tabia zao za uovu."

20-06

Ufalme

Angalia namna ilivyotafasiriwa hapo juu

Walikubali kuwa

Mfalme wa Yuda alilazimishwa kati ya kuhudumia ufalme wa babiloni au uharibiwe

Kuwa mtumishi wa Nebukadneza

Inamaanisha ya kuwa, "Kuiongoza Yuda chini ya Amri ya Nebukadneza."

20-07

Walirudi

Hii inaweza kutafasiriwa kama, "kurudi" au "wakarudi Yuda tena."

Wakauteka Mji

Hii ni kwamba, " wakautawala Mji na watu wake,"

Kunyang'anya

Walichukua vitu vya thamani na kuvipeleka Bebiloni.

20-08

Kuadhibu

Nebukadneza alimuadhibu mfalme wa Yuda kwa kuwaambia askari wake wafanye mambo haya.

Mbele yake

inamaanisha ya kuwa, " ambapo angeona" au " ili kwamba angeweza kuona" au " mbele ya macho yake."

akamfanya kipofu

inaweza kutafasiriwa kama, " akamharibu macho yake."

20-09

Kuacha.... nyuma

Hii ni, " kuwaacha watu masikini waishi Yuda" au "kuwaruhusu watu masikini wabaki Yuda."

kwa kipindi hiki

inaweza kutafasiriwa kama, "ichagua aya inayoonyesha mda mrefu, kwa sababu utumwa ulikaa miaka sabini.

mateka

Neno "mateka" liinamanisha mtu anaondolewa kutoka katika nchi yao kwa nguvu. "Utumwa" ulikuwa ni kipindi cha miaka sabini wakati ambapo waisrael walilazimishwa kuishi Babiloni.

20-10

mateka

Angalia tafasiri kwenye simulizi hapo juu

Hakusahau

Hii ingetafasiriwa kama, " hakupuuza" au " hakumtelekeza" kifungu hiki cha maneno kingeweza kutafasiriwa kama, "aliendelea kudhamini kujitoa kwake kwa watu wake na ahadi zake,"

kulinda

Hii ni "kufanya uangalizi wa karibu"

Ongea nao kwa njia ya manabii

Hii ingetafasiriwa kama, waambie manabii wake ujumbe ambao alitaka kuwaambia wa

20-11

miaka sabini baadaye

Hii inamaanisha baada ya kuwa imepita miaka sabini ya jeshi la Babiloni kuwachukua watu wa Yerusalemu utumwani.

Koreshi

Koreshi pia iliitwa, "Koresha yenye nguvu." Jina "Koreshi" ilimanisha " kama jua" kwa lugha ya Uajemi. kwa sababu Koresha ilikuwa ya kihistoria ingekuwa vyema kutafasiri jina lake, kuliko kutafasiri maana.

Waajemi

Ufalme wa kiajemi ulikua na kumiliki eneo lote kuanzia Urusi ya kati mpka Misri. mahali pake pa kuishi ilikuwa ni sehemu kubwa ya sehemu ya leo iitwayo Irani

Waisrael wakaitwa Wayahudi

Hii ingetafasiriwa kama, kwa sasa watu wa Israel huitwa Wayahudi."

Nchi ya Yuda

Hii ni " Sehemu ambapo Ufalme wa Yuda ulikuwepo kabla ya utumwa.Yerusalemi ulikuwa ni mji mkuu wa Yuda.

20-12

Ufalme wa uajemi

Angalia namna ilivyotafasiriwa hapo juu

Koreshi

Angalia namna ilivyotafasiriwa hapo juu

Yuda

Angalia maelezo kuhusu Yuda kwenye simulizi

kurudi kwa Yuda

kwa sababu Wayahudi wengi walikuwa wana na wajukuu wa wale waliobakia Yuda, hawakuwa wameishi Yuda kabla. Baadhi ya Lugha ingekuwa vizuri kusema, " kwenda Yuda."

mateka

Angalia ambavyo imetafasiriwa kwenye simulizi hapo juu

kurudi

Inamaanisha, " walirudi." Lugha zingine zingependa kusema, "rudi" kwa sababu watu wengi hawakuwa wamewahi kufika Yerusalemu.

20-13

Watu

Hawa ni waisrael, uzao wa Yakobo, ambao kwa sasa wanaitwa Wayahudi.

Ukuta

ukuta huu ulikuwa mpana(2.5 mita) na ulijengwa ili kulinda mji dhidi ya maadui.

walitawaliwa na watu wengine

Hii ni kwamba, " taifa jingine liliwatawala. Wayahudi walitawaliwa na Waajemi wakati ule, na badaye mataifa mengine yaliwatawala.

Kwa nafasi nyingine.

kwenye baadhi ya Lugha hii ingetafasiriwa kama, "sasa" au " kama ambavyo mababu zao walifanya" au " kabla tu ya utumwa."

Waliabudu kwenye Hekalu

Walimwabudu Yawee, yeye aliye Mungu wa kweli, katika hekalu walilojenga.