Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

38-01

Karne nyingi zilizopita

Hii ni, "mamia ya miaka iliyopita" au, "muda mrefu kabla."

38-02

Mtunza mfuko wa fedha za mitume

Hii ni, "wajibika kutunza fedha za mitume" au, "kuwajibika kusimamia mfuko ambao ulikuwa na fedha za mitume na matumizi yake."

Alipenda fedha

Hii ni, "alithamini sana fedha" au, alitaka pesa." Baadhi ya lugha zisingelitumia neno lililo sawa na linaloweza kutumika kwa "kupenda watu."

38-03

Vipande thelathini vya fedha

Kila kipande au sarafu ilikuwa na thamani ya posho ya siku nne.

38-04

Alisherekea

Hii ni, "alikuwa akisherehe"

Alichukua mkate

Hii ingelikuwa inatafsirika kama, "alichukua kipande cha mkate." au " akachukua mkate."

Akauvunja

Baadhi ya lugha zitasema, "akaugawanya vipande" au, "akaugawa nusu yake" au, "akaugawa sehemu yake"

Umetolewa kwa ajili yenu

Hii inaweza kutafsiriwa kwamba, "ambao umetolewa kwaajili yenu"

Fanya hivyo kwa kunikumbuka mimi

Hii ni, "Fanya hivi ikiwa ni njia ya kukukumbusha ambayo Mimi nafanya kwaajili yako." Yesu alikuwa anarejelea kuhusu kifo chake, ambacho kingelitokea karibuni.

38-05

kikombe

Hiki ni, "kikombe cha mvinyo" au, "kikombe kilichojaa kinywaji kilichotengenezwa kwa mzabibu"

Kunywa hiki

Hii ni, "kunywa ambacho kimo katika kikombe hiki" au, "kunywa kutoka katika kikombe hiki." Kunywa katika kikombe chenye zabibu iliyokuwa imetengenezwa ikiwa na rangi nyekundu sana.

Damu ya agano jipya

Hii ingelitafsiriwa kama, "damu inayofanya agano liwezekane." au "damu ambayo ni msingi wa agano jipya."

Imemwagwa

Hii ingelitafsiriwa kama, "itatoka mwilini mwangu" au, "nitatokwa damu."

Kwaajili ya msamaha wa dhambi

Hii ni, "kusudi kwamba Mungu aweze kusamehe dhambi zote za watu kikamilifu."

Nikumbuke

Hii ni, "sherehekea kwa ajili yangu" au, "niadhimisheni." Inaweza pia kutafsiriwa kama, "hasa inayolenga kwangu" au, "jikumbusheni kuhusu mimi."

38-06

Kumpa kipande cha mkate

Hii ni, "kukabidhi kipande cha mkate"

Ni msaliti

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "atanisaliti" au, "yeye ndiye atakaye nisaliti."

38-07

Shetani alimwingia

Hii ni, "shetani alimwingia" au, "akajawa na shetani."

Yuda aliondoka na akaenda

Lugha nyingine inaweza kupendelea kusema, "Yuda alikiacha chakula na akaenda." au, "Yuda aliondoka ndani na akaenda nje."

38-08

Mlima wa Mizeituni

Hili ni jina mlima uliofunikwa na miti ya mizeituni, nje tu ya jiji la Yerusalemu. Pia inaweza kutafsiriwa kama, "mlima wenye miti ya mizeituni."

kuniacha

Hii ni, "kunitenga mimi" au, "kuniacha."

Imeandikwa

Hiyo ni, "Imeandikwa kwenye neno la Mungu" au, "imeandikwa katika maandiko" au, "Mmoja wa manabii aliandika." Pia inawezekana kusema, kilichoandikwa kitatokea." au, "itatimia kama ilivyoandikwa." Unabii huu unarejelea kifo cha Yesu na wafuasi wake kukimbia.

Nitampiga

Hii ni, "Nitaua"

mchungaji na kondoo wote

Usitumie jina la Yesu katika nukuu hii kwa sababu nabii aliyeandika mwanzoni hangelijua jina la mchungaji. Pia usirejelee wanafunzi kuwa ni wanafunzi. Inafaa sana kutumia maneno yenye maana ya "mchungaji" na "kondoo" unapotafsiri.

watatawanyika

Hii ni, "kwenda huko na huko kwa uelekeo tofauti"

38-09

Sitakuacha

.........

Kuwa nanyi wote

Hii ni, "kuwatawala kikamilifu" au, "anataka ninyi mtumike kwake kikamilifu." Neno wewe au "ninyi" ni wingi katika kauli hii. Maneno haya "wewe" na "yako" yanayofuata yako katika umoja.

Imani yako haitashindwa

Hii ni, "kwamba hutaacha kuniamini"

Kabla jogoo hajawika

Kwa kawaida jogoo huwika kabla ya kuanza siku mpya. Kama hiyo haijaeleweka , itasaidia kusema, "kabla ya kuwika jogoo mapema kesho" au, "kabla hajawika jogoo kesho asubuhi."

38-10

Kukukana

Hii ni, "nakujua lakini nakana" au, "mimi mwanafunzi wako halafu nakana" au "nakukataa"

38-11

Sehemu inayoitwa Gethmane

Hii ingeliweza kutafsiriwa, "eneo jirani lililoitwa Gethsemane" au, au "sehemu iliyoitwa Gethsemane chini ya Mlima wa Mizeituni."

Kuingia majaribuni

Hii ni, "wasingetenda dhambi walipojaribiwa" au, "Wasingeliingia kwenye majaribu yaliyokuwa yanaelekea kuwapata."

Peke yake

Hii ingetafsiriwa kama "yeye tu."

38-12

Kunywea kikombe cha mateso

Hii ni, "kupitia amateso haya" au, "kuteseka kwa kinachokaribia kutokea" au, "kuvumilia haya mateso."

Mapenzi yako yafanyike

maelezo haya yanamaanisha, "fanya ambacho umepanga" au, "fanya unachohitaji kufanya."

38-13

Kila baada ya maombi

Hii ni, "Kila wakati Yesu aliomba maombi hayo." Hii inarejelea zile mara tatu aliomba kama ilivyotajwa

38-14

Akaja

Lugha zingine zitapendelea kusema, "akaenda"

Salaam

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "habari" au, "amani" au, "Habari za mchana."

Ishara

Hiki ni, "kiashiria."

Unanisaliti mimi kwa busu

Hii ni, "ni hakika unakwenda kunisaliti mimi kwa busu?" Yesu hatafuti jibu kwenye swali hili. Hivyo lugha zingine zingelitafsiri kama ifuatavyo: "unanisaliti kwa kunibusu!" au, "unafanya usaliti mbaya wa kunibusu kabisa."

38-15

Ikawa askari walimkamata Yesu

Hii ni, "wakati askari walikuwa wakimkamata Yesu."

Aliuvuta upanga wake

Hii ni, "kutoa upanga kutoka mahali alipokuwa ameuweka."

Lazima nimtii Baba yangu

Hii ni, "Sitafanya hivyo kwa sababu lazima nitii mapenzi ya Baba yangu, niko tayari kukamatwa."