Kiswahili: Open Bible Stories Translation Notes

Updated ? hours ago # views See on DCS Draft Material

47-01

kutangaza

Hiyo ina maana kwamba, "kufundisha" au, "kuhubiri."

mfanyabiashara

Hii ingeweza kutafsiriwa kama, "muuzaji" au, "mmiliki wa biashara" au, "mwenye biashara."

47-02

aliufungua moyo wa Lidia

Hii ina maana kwamba, "alimwezesha Lidia"

yeye na familia yake walibatizwa

Hii pia inaweza kutafsiriwa kama, "walimbatiza Lidia na familia yake."

hivyo wakakaa naye yeye na familia yake

Hii ilikuwa desturi ya kawaida siku zile kwa watu kuwakarimu wageni nyumbani mwao. Kulikuwa hakuna nia mbaya kinyume cha maadili katika kufanya hivi.

47-03

waliomtumikisha

katika hili, hii inaweza pia kutafsiriwa kama, "wamiliki wake" au, "watu wanaommiliki"

kama mtambuzi

Hiyo ina maana kwamba. "ni kama mtu anaye waambia watu yale ambayo yangewatokea katika siku zao za usoni."

47-04

njia ya kupata wokovu

Hiyo ina maana kwamba, "ni jinsi unaweza kuokoka" au, " jinsi gani Mungu anaokoa watu" au. "Mpango wa Mungu kuwaokoa watu"

47-05

siku moja

Hii sentensi inatambulisha tukio ambalo limetokea huko nyumba, lakini haisemi ni wakati gani hasa. Lugha nyingi zinanamna kama hiyo ya kuanza kuhadithia hadithi.

aligeuka kwake

Hii ina maana kwamba, "aligeuka na kumwangalia"

kwa Jina la Yesu

Hiyo ina maana kwamba, "kwa mamlaka ya Yesu." Kwa sababu ya mamlaka ya Yesu, Paulo aliweza kuamuru pepo kuondoka.

toka ndani yake

Hiyo ina maana kwamba, "muache" au, "nenda mbali naye"

47-06

bila ya pepo

Hiyo ina maana kwamba. "bila ya nguvu kutoka kwa pepo" au, "sasa kwamba hakuwa na pepo."

wakati ujao

Hiyo ina maana kwamba, "mambo yatakayowatokea katika wakati ujao."

Hii ilimaanisha kwamba

Hii ingeweza pia kutafsiriwa kama, "Kwa sababu ya hili" au, "Kwahiyo."

47-07

kuwatia

Hiyo ina maana kwamba, "kuwaweka."

47-08

usiku wa manane

Hii ingeweza kutafsiriwa kama, "usiku sana" au, "alfajiri mapema sana." Hii ilikuwa wakati ilipokuwa giza kabisa huko nje, ambapo watu kwa kawaida wanakuwa wamelala."

wakiimba nyimbo za kumsifu Mungu

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "kumsifu Mungu kwa kuimba" au, "kuimba nyimbo za kumsifu Mungu" au, "kuimba nyimbo ambazo zinampa Mungu sifa."

47-09

kuwa wazi

Hiyo ina maana kwamba, "kutokufungwa na ghafla kuwa wazi kabisa."

kuanguka

Hiyo ni maana kwamba, "ghafla ilitoka" au, "ghafla ikajitenga hivyo wafungwa wakawa wamefunguliwa."

47-10

Askari mlinzi wa wafungwa

Hiyo ina maana kwamba, "afisa mwangalizi wa gereza."

Sisi

Baadhi ya lugha zinaliangalia neno "sisi" kimaalum kabisa ambayo haimhusishi mtu anayeongeleshwa. Hapa "sisi" haimuhusishi askari mlinzi wa wafungwa, ni Paulo tu pamoja na wafungwa wengine.

47-11

kusalimika

Hii ingeweza kutafsiriwa pia kama, "ili niweze kuokoka kutoka katika dhambi zangu" au "ili kwamba Mungu aniokoe kutoka katika dhambi zangu." Swali linahusu wokovu kutoka katika kuadhibiwa na Mungu aliyesababisha tetemeko.

Mwamini Yesu, Bwana mkubwa.

Hii inaelezwa kwa wote wawili yaani askari mlinzi wa gereza pamoja na familia yake, ambao wote walikuja kuamini na kubatizwa. Baadhi ya lugha zingetumika kuonyesha kwamba Paulo anaongea na kundi.

wewe na watu wa nyumbani mwako mtapata wokovu.

Hii inaweza kutafsiriwa kama, "Mungu atawaokoa wewe na familia yako kutoka katika adhabu ya milele kwa sababu ya dhambi zenu." Hakikisha kwamba wokovu unaoongelewa hapa ni wakiroho, na si wa kimwili.

47-13

viongozi wa mji

Hii inaelezea juu ya, "maafisa wa mji" au, "mamlaka ya mji."

Injili ya Yesu iliendelea kuenea

Hiyo ina maana kwamba, "Watu katika maeneo mengi zaidi walikuwa wakisikiliza habari njema kuhusu Yesu."

Kanisa liliendelea kukua

Hiyo ina maana kwamba, "watu wengi zaidi walikuwa wanakuwa sehemu ya kanisa" au, "watu wengi zaidi na zaidi walikuwa wakimwamini Yesu."